Nội dung text Grade 1-3 Kiswahili - Revised.pdf
TAASISI YA UKUZAJI MITAALA KENYA JAMII ADILIFU NA YENYE UJUZI KISWAHILI MAZOEZI YA LUGHA MTAALA WA SHULE ZA MSINGI GREDI YA 1, 2 NA 3
ii Chapisho la Kwanza 2017 Chapisho la Pili 2024 Haki zote zimehifadhiwa. Hairuhusiwi kuiga, kunakili, kupiga chapa au kutoa mtaala huu kwa njia yoyote ile bila idhini, kwa maandishi, ya mchapishaji. ISBN: 978-9914-43-071-4 Kimechapishwa na kutolewa na Taasisi ya Ukuzaji Mitaala Kenya
iii DIBAJI YA WAZIRI WA ELIMU Serikali ya Kenya imejitolea kuhakikisha kuwa malengo ya sera ya elimu, mafunzo na utafiti yanatimiza maazimio ya Katiba ya Kenya, 2010, Ruwaza ya Kenya, 2030, Sera ya Mtaala ya Kitaifa ya 2019, Malengo ya Maendeleo Endelevu ya Umoja wa Mataifa na mikataba ya kieneo na kimataifa ambayo Kenya ni mshirika. Katika kutimiza kauli mbiu ya Elimu ya Msingi, Wizara ya Elimu imefanikiwa kuanzisha utekelezaji wa Mtaala wa Kiumilisi katika viwango vya Chekechea, Shule za Msingi na Shule za Junia. Utekelezaji wa Mtaala wa Kiumilisi unahusisha ufuatiliaji na tathmini ili kuhakikisha kwamba umefanikiwa. Baada ya kutekelezwa kwa mtaala huu kwa awamu ya kwanza ya miaka mitano, tathmini tamati ya utekelezwaji huu ilifanywa ili kubaini iwapo matokeo yanayotarajiwa kama yanavyoelezewa katika Utaratibu wa Mtaala wa Elimu ya Msingi (BECF) yalifikiwa. Serikali ya Kenya iliunda jopokazi ya Rais ya: Presidential Working Party on Education Reforms (PWPER) mwaka wa 2022 kushughulikia masuala nyeti yanayotatiza sekta ya elimu. Jopokazi hii ya rais ilitoa mapendekezo mbalimbali yanayoathiri elimu nchini yaliyochochea kutazamwa upya kwa mtaala wa elimu. Mapendekezo ya jopokazi hii, ripoti za kuangalia utekelezaji wa mtaala, ripoti za tathmini tamati kuhusu utekelezwaji wa elimu ya msingi kiawamu na taarifa kutoka kwa wanaotekeleza mtaala na washikadau wengine zilichangia usawasishaji na kutazamwa upya kwa mtaala wa elimu ya awali. Mtaala uliofanyiwa marekebisho wa shule za msingi unatoa nafasi kwa wanafunzi kukuza uwezo wa kusoma na kuandika pamoja na mbinu za kuweza kuhesabu (basic literacy and numeracy) na kuweza kuingiliana na mazingira yao. Wanafunzi wanajenga juu ya umilisi walioupata katika shule za chekechea na pia kuwaandaa kujiunga na shule ya msingi ya juu. Mtaala unawasilisha Malengo ya Elimu ya Taifa, Matokeo yanayotarajiwa ya kiwango, kauli kiini, matokeo ya kijumla yanayotarajiwa, mada na mada ndogo. Mtaala pia unatoa matokeo maalum yanayotarajiwa, shughuli za ujifunzaji zilizopendekezwa, maswali dadisi yaliyopendekezwa, umilisi wa kimsingi, masuala mtambuko, maadili na pia viwango na vigezo vya kutathmini. Ni matumaini yangu kwamba mitaala hii itatumiwa na mashirika ya serikali na washikadau wengine kupanga kikamilifu na kutekeleza wa Mtaala wa Kiumilisi. HON. EZEKIEL OMBAKI MACHOGU, CBS WAZIRI WA ELIMU WIZARA YA ELIMU
iv DIBAJI YA KATIBU MKUU Mwaka wa 2019 Wizara ya Elimu ilizindua utekelezaji wa Mtaala wa Kiumilisi kupitia mfumo wa ana kwa ana. Daraja ya chini ya Shule za Msingi ni kiwango cha kwanza katika elimu ya msingi baada ya masomo ya Chekechea katika muundo uliotolewa katika Basic Education Act of 2013. Mitaala iliyofanywa upya imejengwa katika msingi wa elimu ya Chekechea. Inawapatia wanafunzi nafasi ya kuingiliana na mazingira yao pamoja na kukuza mbinu za kusoma, kuandika pamoja na kuhesabu. Hii inaoana na ruwaza na mwito wa mageuzi ya mtaala kama inavyoelezwa katika Mtaala wa Kiumilisi. Kiwango hiki cha elimu ni muhimu katika kuchangia kufikia ruwaza na mwito wa mabadiliko yanayoendelea ya kimtaala kama ilivyoelekezwa katika Mswada Elekezi Nambari 1 wa mwaka 2019 kuhusu Katika kuafikia elimu na mafunzo yenye ubora na jumuishi kwa maendeleo endelevu nchini Kenya. Mswada Elekezi huo unaeleza kuhusu kuvuka kutoka mtaala wa Kimafunzo na kuzingatia kukuza vipawa vya kila mwanafunzi Mitaala ya shule za msingi daraja ya chini katika juzuu tatu: Juzuu ya kwanza: English Language Activities na Kiswahili Mazoezi ya Lugha. Juzuu ya pili: Indigenous Language Activities na Creative Activities. Juzuu ya tatu: Mathematical Activities, Environmental and Religious Activities. Mitaala hii inalenga kukuza umilisi wa mwanafunzi kwa kutoa maelezo yanayooana na mihimili ya Mtaala wa Kiumilisi. Mitaala hii pia inalenga kuelekeza wasomi kwa njia ifaayo na kusaidia ujifunzaji ili kuwasaidia wanafunzi kufikia matokeo yanayotarajiwa. Inatoa mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji za kimwingiliano ili kufanya ujifunzaji uwe wa kupendeza, kisisimua na kuburudisha. DKT. BELIO KIPSANG KATIBU MKUU IDARA YA SERIKALI YA ELIMU YA AWALI NA ELIMU YA MSINGI WIZARA YA ELIMU